UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Wednesday, April 11, 2012

TODAY'S MESAGE-A FOOD OF SOUL

 Efforts and courage are not enough without purpose and direction,
ahead on this Do not let the hero in your soul perish to fulfil the said,
Check your road and the nature of your battle n believe that you are a
high achiever. The world you desired can be won. It exists, it is real,
it is possible, it is yours

with regards
japhet

Tuesday, April 3, 2012

TAARIFA YA KIKAO CHETU CHA CHAMA KILICHOFANYIKA 001.04.2012

Habari zenu wanachama,

Nichukue fursa hii kutoa shukrani zangu za pekee kwa wanachama wote kwa moyo wenu na suhirikiano mnaoendelea kutupa katika kusukuma gurudumu hili lililo mbele yetu, ni kazi kubwa inayohitaji moyo lakini inatupa hamasa sisi kama viongozi kwa sababu moja tu, ushirikiano mnaotoa kwetu, ni jambo la kupendeza na kumshukuru Mungu pia.

Rejea na kichwa cha habari hapo juu, kikao chetu kilifana sana na mambo kadha wa kadha tuliyajadili na kufikia muafaka na mengine bado hatujafikia muafaka ingawa michakato bado inaendelea na tutaendelea kutoa taarifa za kiutendaji kadri tutakavyoweza na kadri mwenyezi Mungu atakavyotusaidia.

Ajenda kuu ilikuwa ni kujadili mabadiliko makubwa ya katiba na kupokea mapendekezo ya wanachama kwa njia ya mjadala kwani suala hili lilipewa muda mwingi kwa sababu ya upana wake na mwisho tulikubaliana mambo mengi ikiwa ni pamoja na

1. Uongozi utakaochaguliwa utatoa huduma kwa kipindi cha miaka miwili
2.Suala lolote la chama linalotakiwa kuamriwa kwa njia ya kura lazima liungwe mkono na theluthi mbili ya wanachama
3.Mkutano mkuu utakuwa halali iwapo utaudhuriwa na theluthi mbili ya wanachama wote
4.Sababu zitakazokubaliwa za mtu kutofika ni Ugonjwa, kuwa nje ya mji kikazi au dharura yoyote ile inayokubalika kulingana na uzito wake utakavyokuwa na taarifa zitumwe kwa katibu mapema sio chini ya masaa 6 kabla ya mkutano.


Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo kimsingi tumeafikiana ikiwa ni pamoja na kupitsisha mabadiliko makubwa ya katiba,

Vilevile suala la kusajili chama linaendelea vizuri na jambo la msingi lililotuchelewesha ni katiba, lakini kwa sasa nadiriki kusema kuwa muda si mrefu tutafikia hatua nzuri kwani katiba ilikuwa lazima ikidhi vigezo vya wizara ya mambo ya ndani.

Katiba imetamka wazi kuwa kuna mambo ambayo hayajatajwa kwenye katiba ila chama kitakuwa na sheria ndogondogo (by laws) ambazo zitasaidia kusimamia na kutoa uelekeo wa shughuli za chama.

Mwisho niwakumbushe kujitokeza kwa wingi siku ya 14.04.2012 ambapo chama tutajumuika pale msasani club na utaratibu mzima utatolewa na viongozi wa kamati husika kama tulivyokubaliana.

Nawashukuruni nyote na mungu awabariki
Imetolewa na Japhet Mukala
Mwenyekiti wa chama
03.04.2012