UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Sunday, June 3, 2012

MATUKIO YALIYOJIRI KWA KIPINDI CHA MWEZI MMOJA ULIOPITA HADI LEO 03062012

Ndugu wanachama,

kwanza kabisa nawasalimu, ninayo imani kuwa mu wazima na mnaendelea vizuri na shughuli zenu za ujenzi wa taifa na chama chetu kwa ujumla,

Pili ningependa kutoa taarifa fupi juu ya matukio yaliyojiri kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita kama ifatavyo

1.Tukio la kwanza lilikuwa ni kwenda kumpa pole dada Jacqueline Kahembe aliyepata ajali, niwashukuru sana wale wote waliojitokeza kwa moyo wenu mliounesha, ni kweli Jacque kaumia sana na anahitaji sara, Mungu amatangulie katika kipindi hiki kigumu sana kwake na sisi kama vijana tupo nyuma yake.

2. Tukio la pili lilikuwa kwenda kumsalimia ndg yetu Stanley Pesha, aliyefiwa na mama yake mzazi, vilevile  nichukue fura hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa moyo mliounesha, huo ndo utu na maana halisi ya jumuiya kama hii tuliyonayo! hikika ni jambo jema na la kupendeza sana. ninachowaomba, ni kuendelea kumtia moyo kaka yetu katika kipindi hiki kigumu sana kwa kuondokewa mtu muhimu sana katika maisha yetu ya hapa duniani.

3.Tukifanya get together event, ilikuwa na shughuli nzuri na kweli ilifana sana, nawashukuru sana kwa kujitokeza na kujumuika na wanchama wengine ktk hafla hiyo iliyofanyika msasani beach club!

4. Ndugu yetu bwana Fortunatus Byashalila na mkewe walibahatika kubarikiwa mtoto wa kiume, Mungu ni mwema sana na chama kinatoa salam za pongezi kwa kupata mwanafamilia mwingine ndani ya umoja wetu, mtoto wetu kwa sasa anaumwa na amelazwa hospitali ya muhimbili na baba mzazi alinihakikishia kuwa afya yake kwa sasa ni nzuri na wanategemea kuachiwa kesho yani tarehe 05.06.2012 siku ya jumanne. Tuungane na familia ya Byashalila kumuombea mtoto wetu apone haraka.


Mwisho ni washukuru sana kwa ushirikiano ambao mmekuwa mkiutoa katika ujenzi wa chama
Imetolewa leo 04062012 na
japhet Mukala
Mwenyeki wa chama