UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Wednesday, October 10, 2012

MKUTANO MKUU WA CHAMA ULIOFANYIKA 07102012

Habari zenu wapendwa,

Kwa niaba ya chama napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wanachama wote waliojitokeza katika mkutano wetu mkuu wachama, tulijadili mengi sana na siku hiyo agenda kuu zilikuwa
1.Ripoti ya mweka hazina
2.Ripoti ya utendaji iliyowasilishwa na mwenyekiti wa chama aliyemaliza mda wake
3.Mabadiliko ya katiba
4.Mwenendo wa chama kwa ujumla

Niwashukuru sana kwa michango yenu ya kimawazo katika ajenda zilizoletwa, ni dhahiri kuwa zipo ajenda ambazo tulishindwa kuzijadili kutokana na muda kuwa mchache na zingine tulizijadili na makubaliano yalifikiwa, taarifa ya mwenyekiti ya utendaji na ya mweka hazina, zote zilitoa mapendekezo ambayo yote kwa pamoja hatukuyajadili kwa mapana yake ingawa tutayatengea muda wa kuyajadili na kufikia makubaliano.

Mwenyekiti wa chama alivunja rasimi uongozi uliokuwepo kwa mujibu wa katiba na kuitisha uongozi mpya ambao kimsingi utafanyika kwa mujibu wa katiba mwezi ujao ukisimamiwa na kamati maalum iliyocteuliwa kufanya mchakato mzima wa uchaguzi.

Suala la msingi ni kuomba wale wote wanaodhani wanawiwa kukitumikia chama wanaombwa kuchukua fomu za kugombea uongozi kwani nafasi zote sita zipo wazi kwa sasa. uongozi ni dhamana na si cheo. tujitoa na kuonesha uzalendo kwa kusaidiana katika mchakato mzima wa kupata viongozi wanaofaa kwani uongozi ndo injini ya chama.

Tuna imani hili litafanyika kwa ufasaha na chama kitapata viongozi wake ambao watakuwa dira ya chama katika kukamilisha malengo yetu tuliyojiwekea.

Nawashukuru sana
na Mungu wabariki

Imetolewa na
Japhet Mukala