UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Tuesday, May 22, 2012

SALAMU ZA PONGEZI

Natumaini mu wazima wa afya,

Kwanza nichukue fursa hii kumshukuru mwenyezi Mungu kwa yote anayotutendea, Mungu yu mwema siku zote na hakika anatupenda,

Pili nichukue fursa hii kutoa salam na shukrani zangu za pongezi kwa wale wote waliojitokeza ktk party yetu iliyofanyika 19052012,shukrani za Kipekee ziwaendee Joymetta na Hamza kwa jitihada zao za dhati kabisa kufanikisha jambo hilo, sherehe ilikuwa nzuri sana, ni mwanzo mzuri sana na nina uhakika suala hili limetoa uhamsho wa kipekee miongoni Mwetu!

Tuzidi kushirikiana katika kujenga chama!
Mungu awe nasi na abariki kazi ya mikono yetu!
Imetolewa na Japhet Mungu
22052012

Wednesday, May 9, 2012

TAARIFA YA KIKAO CHA TANO KWA MWAKA 2012

Kwanza nichukue fursa hii kuwasabahi, pili nitoe shukrani zangu za kipekee kwa wale wote wenye nia ya dhati na walijitokeza hata wale ambao hawakujitokeza ila walitoa taarifa zao katika njia sahihi za utoaji wa taarifa,

Ni mambo meingi sana yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na kupata taarifa kutoka kwenye kamati inayoshughulikia usajili wa chama, hatua iliyofikiwa ni nzuri, na mambo ambayo yamebaki ni barua ya utambulisho toka kwa mkuu wa wilaya, wasifu wa viongozi, pamoja na gharama zote ambazo ni takribani tzs 150,000.00.

Vilevile tulijadili umuhim wa kutilia maanani malengo makuu ya chama, chama ni cha wote hivyo kila mtu anao wajibu wa kuhakikisha tunasonga mbele na yale tunayokubaliana yanazingatiwa kwa uzito wake, hili ni jambo la muhim sana kwani ndo limetuunganisha na kuwa familia moja yenye lengo la kukuza upendo na mshikamano miongoni mwa wanachama. Kama uongozi, hili tutalisema na kulihubiri kila wakati ili kiloa mmoja wetu aelewe dhima halisi ya uwepo wetu na nini wajibu wetu pamoja na mipango yetu.

Vilevile tulijadili suala la kuharisha kwa shughuli yetu na sababu zilikuwa wazi, mawazo mengi yalitolewa baadhi wakisema tuhairishe kabisa wengine wakisema hapana, kama ilivyo ada yetu, chama kinaendeshwa kwa misingi ya kidemokrasia, mawazo mengi yaliamua hili lifanyike 19.05.2012 na lilikubaliwa hivyo. kwa maana hiyo basi siku hiyo 19052012 tutakuwa na event yetu kama tulivyokuwa tumeitangaza hapo mwanzo, mahali ni palepale, muda na maelezo mengine yatatolewa na viongozi husika.

Maazimio mengine yatatolewa/yameshatolewa na katibu mkuu wa chama kwa njia yetu ya kawaida!

niwapongeze sana na kuwatakia shughuli njema za ujenzi wa taifa letu!
kazi ni utu wa mwanadamu
tuuchukie unyonyaji na ufisadi bali tuhimize zaidi uwajibikaji wa kweli!
Tukifanya hivyo tutakuwa tumejitendea haki sisi wenyewe pamoja na taifa letu!

Imetolewa na Japhet Mukala
Mwenyekiti wa chama.