UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Friday, July 13, 2012

TAARIFA KWA WANACHAMA WOTE

Kwanza kabisa napenda kuwasalimia

Nichukue fursa hii kuwapa pole na majumu yenu ya kila siku ya ujenzi wa Taifa na chama kwa ujumla, chama hadi sasa kinaendelea vizuri na tunamshukuru Mungu.

Rejea kikao chetu cha mwezi huu, nawashukuru sana wanachama wote waliojitokeza hata ambao hawakufanya hivyo lakini walitutaarifa juu ya kutoudhuria kwao, kikao kilianza mapema saa kumi na nusu na mambo mengi sana yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na Taarifa ya utendaji ya miezi sita iliyopita kutolewa na mwenyekiti wa Chama. baadhi ya mambo yafuatayo yalijadiliwa

1.Maudhurio ya wanachama hayaridhishi na hili tutalitolea ufumbuzi kwa kikao kijacho
2. Tulijadili juu ya watu wote ambao wanadaiwa na chama na barua juu ya madai zilitumwa kwa kila mwnachama anayedaiwa kuanzia shillingi moja na kuendelea
3.Tulikubaliana kuchukua maamuzi mazito ambayo tutayafanya kutokana na majibu ya barua tulizotuma kwa wanachama wenye matatizo mbalimbali kichama, na hayo maamuzi ya kamati kuu yatabarikiwa na wanachama kwenye mkutano wa mwezi wa nane.
4.Tulikubaliana pia kuwa siku ya jumapili yanai 15.07.2012 tutaenda kuwatembelea watoto yatima, nawashukuru wale wote waliojitolea kwa moyo kwa ahadi zao za mali na pesa
5.Tulikubaliana moja ya agenda za kikao kijacho ni kujadili juu ya kutafuta walezi wa chama kwani wale wote tulio walenga imeonekana wamezidiwa na majukumu

.haya ni baadhi tu ya yale tuliyoyajadili.
kwa taarifa zaidi itatolewa na katibu mkuu wa chama
Japhet Mukala

No comments: