UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Monday, July 16, 2012

SHUKRANI ZA KIPEKEE KWA KUFANIKISHA SAFARI YA KUWAONA WATOTO YATIMA.


Poleni na majukumu wadau,

Napenda kuchukua fursa hii, kutoa shukrani zangu za dhati kutoka moyoni kwa wale wote waliojitokeza jana kwenda kuwaona wadogo zetu, vilevile nawashukuru wadau wengine ambao wameshiriki nasi kwa njia ya michango pamoja na kuwa mbali na Dar es salaam, vilevile sitawasahau wale wote walioshindwa kufika ila wametuma uwakilishi wao kwa namna nyingine,

Ni jambo la kumpendeza Mungu sana kw...a tukio la jana, nimshukuru Mungu sana na aendelee kututia moyo katika kuyafanya haya kwani hakuna wa kumwachia zaidi yetu sisi na wewe pia.

Naushukuru sana uongozi wa kutuo kwa ukarimu wao kwetu na niwashukuru wadogo zetu pia kwa jinsi walivyokuwa wakarimu sana kwetu,ni kweli bado jitihada za hali na mali zinahitajika sana katika kuyakamilisha haya!hakika tutafika.

Niwatakie kazi njema na Mungu awabariki pale mlipotoa awaongezee

No comments: