UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Tuesday, January 31, 2012

MIKUTANO YA CHAMA KIKATIBA


                 10. Chama kitakuwa kinafanya mikutano ya aina tatu (3)
                       kama ifuatavyo.

10.1.Mikutano ya kila jumapili ya mwanzo wa mwezi ambayo itakuwa imelenga zaidi kuwa na mawasiliano ya karibu kati ya mwanachama na mwanachama na kuangalia lipi lifanyike ndani ya chama ili kuleta ustawi imara na kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha chama

10.2 Mikutano ya kila robo ya mwaka itakayopitia mwenendo wa chama kwa kila robo mwaka na kufanya marekebisho ipasavyo au kutoa mapendekezo ya nini kifanyike kutoka kwa wanachama.

10.3. Mkutano wa dhararu ambao utawahusisha wanachama wote au kamati ya uongozi pindi itakapobidi kuwa hivo na hii itatokana na jambo ambalo litakuwa mbele yetu na kudhibitishwa na mwenyekiti wa chama.

Mahali pa kukutana ni TP MAZEMBE, iko nyuma ya ubungo plaza karibu sana na uwanja wa mpira, na muda ni saa tisa na nusu hadi kumi na mbili na nusu. mwanachama mwenye ajenda binafsi ili ijadiliwe na wanachama inatakiwa uwasilishwe kwa katibu mapema ili uongozi upate muda wa kuiangali umuhim wake na kuitolea ufafanuzi.

Mgeni aliye alikwa hatakuwa na fursa ya kujadili hoja au ajenda iliyoletwa mezani hadi pale atakaposajiliwa kama mwanachama kamili ingawa anaweza kupewa nafasi ya kushauri.

KARIBU KWENYE MKUTANO WETU 05.FEB.2012

Ndugu wanachama,

Mnakumbushwa kuudhuria mkutano wetu wa kikatiba siku ya jumapili eneo letu la kila siku pale ubungo!mada muhimu ni malengo ya mwaka huu, unaombwa kuwahi sana muda ni saa tisa jioni hadi saa kumi na mbili!kufika kwenu ndo mafanikio ya chama!
mkaribishe na mwenzako pia!

imetolewa na
Japhet Mukala

Monday, January 30, 2012

TANZIA

Kwa niaba ya chama, napenda kutoa salam za pole kwa ndugu yetu bwana Mbaraka Nyaigesha kwa kuondokewa na baba yake mkubwa, msiba umetokea jana huko mbeya ila mipango ya mazishi inafanyika ubungo kibangu! kwa wale wote watakaoweza naomba tukutane ubungo riverside saa kumi jioni ili twende kumpa pole!
kazi ya mola kamwe haina makosa, tumshukuru kwa kila jambo!
bwana ametoa na bwana ametwaa,
jina lake lihimidiwe
imetolewa na Japhet Mukala

Friday, January 20, 2012

SALAMU ZA PONGEZI

Kwa niaba ya chama cha vijana wa kanyigo waishio Dar es salaam, napenda kutoa shukrani za pongezi kwa bwana Dickson Nestory na mkewe kwa kubarikiwa mtoto wa kike leo alfajiri, afya za mama baba na mtoto zinaendelea vizuri, tunapenda kumtakia mtoto wetu maisha mema na marefu yenye baraka tele.


imetolewa na Japhet Mukala
mwenyekiti wa chama

Sunday, January 15, 2012

YALIYOJIRI KIKAO CHA 08012012

Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kuwashukuru wanachama wote waliojitokeza kwenye kikao chetu , yapo mengi yaliyojiri na zaidi tulitembelewa na mwl Boniphace Kahembe, alitoa nasaa zake na chama tulizipokea kwa mikono miwili,

Baadhi ya mambo tuliyokubaliana kwenye kikao chetu cha 08 jan 2012

1. Aprial tutakuwa na study tour ya bagamoyo na hamza pamoja na Joymetta walipewa jukum la kufanya tathmini ya safari nzima, ripoti yao itasomwa kikao kijacho cha mwezi february.
2. Wajumbe wote walishirikishwa kuchangia mawazo kwa njia ya maandishi juu ya nini kifanyike ndani ya kipindi cha 2012 na yatapitiwa na kamati ya uongozi, hivo majumuisho yote yatatolewa kikao kijacho cha mwezi february
3.Tulikubaliana kikao kijacho wanachama watapewa namba za uanachama ila kwa wale walijaza fomu zao vizuri na kuweka passpot size kama ilivyooagizwa na uongozi wa juu.
4. Juvenali alitoa ufafanuzi wa vijwanja kama alivyoagizwa na chama na wito ulitolewa kwa wanachama ambao wako tayari kununua wawasiliane nae,
5. Tulikubaliana kuwa kila mwaka tutakuwa tunafanya study tour mara mbili, mapendekezo ya lini na lini yatatolewa ufafanuzi kikao cha mwezi february.
6. Mkutano wa kimkakati wa kupanga malengo ya chama utakuwa unafanyika december kila mwaka baada ya uchaguzi wa viongozi, na hii ni kutoa fursa kwa uongozi mpya kupanga malengo yao na kutafuta njia iliyo nzuri zaidi ya kutekeleza katiba, vilevile ni kutoa muda mzuri wa chama kuanza mwaka na malengo tayari yanajulikana kwa wanachama.

imetolewa na japhet mukala