UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Wednesday, March 28, 2012

UNAKARIBISHWA KWENYE KIKAO CHA CHAMA 01.04.2012

Ndugu mwanachama,

Nipende kuchukua fursa hii, kuwakaribisha kwenye kikao chetu cha chama cha kila jumapili ya mwanzo wa mwezi, kikao kchetu kitakuwa na mambo mengi ya kujadili na zaidi kitajikita kwenye mabadiliko makubwa ya katiba ambayo yamefanywa na uongozi wa chama uliopewa na baraka na wanachama kufanya hivyo ikiwa ni katika harakati za kuafanya usajili wa chama kisheria, pili tutajadili kidogo juu ya trip yetu tunayotakiwa kuifanya 14.04.2012 kama tulivokubaliana,

Muda wa kikao ni uleule saa kumi kamili kikao kitaanza na mahali ni TP Mazembe ubungo plaza, nawakaribisha nyote, chama ni chetu kwa ajili ya maendeleo yetu.

Imetolewa na
Japhet Mukala

Monday, March 19, 2012

TAARIFA FUPI YA KIKAO CHA VIONGOZI WA CHAMA

habari za weekend wadau!

Rejea makubalianao ya kikao cha chama kilichopita, jumamosi tulifanya kikao cha viongozi wa chama, mambo mengi yalifikiwa muafaka ambayo ni pamoja na kufanya marekebisho ya katiba, ni mabadiliko makubwa sana tumeyafanya ili tuwe na katiba nzuri yenye kukidhi matakwa ya sasa na baadae ya chama, kiako kilianza sa 10.30 na kumalizika sa 12.30, maazimio ya kikao yote yataelezewa siku ya 01.04.2012 ambapo tutafanya mkutano wa chama wa mwanzo wa mwezi! nawatakia kazi njema za ujenzi wa taifa!

Imetolewa na
Japhet Mukala

Monday, March 12, 2012

SHUKRANI KWA WOTE WALIOJUMUIKA NASI KWENDA KUMPONGEZA MAULID ABDALLAH

Nichukue fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa wale wote waliojitokeza kwenda kumtembelea na kumpongeza Bwana Maulid Abdallah na famila yake kwa kupata mtoto, ni jambo jema na la kufurahisha kwa moyo mliouonesha, maudhurio yalikuwa ya kuridhisha na Maulid pamoja na familia yake wanashukuru sana kwa upendo tuliouonesha,zaidi niwatakie afya njema na tuendelee na moyo huo katika siku za usoni!

Mungu awabariki wote
Japhet Mukala
12.03.2012

Monday, March 5, 2012

TAARIFA YA MKUTANO WA CHAMA ULIOFANYIKA 04.03.2012

Kwanza kabisa nichuke nafasi hii kuwashukuru wale wote waliojitokeza kwenye mkutano wa jana na hata wale walioshindwa ila walitoa taarifa juu ya kutofika kwao!

Mkutano wetu wa jana ulikuwa na manufaa mengi sana kwani mambo muhim sana kwa uhai wa chama yalijadiliwa na kufikiwa muafaka, niwapongeze wote waliotoa michango yao kwa njia mbalimbali,

baadhi ya mambo amabayo chama kinatakiwa kuyafanyia kazi ni kama yafuatayo.;-

1.Kufanya marekebisho ya katiba ili kukidhi vigezo vya chama cha kijamii kwa mijibu wa wizara ya mambo ya ndani ikiwa ni harakati za kusajili chama chetu kitambulikane kisheria
2.Kuandaa safari yetu tuliyopanga kuifanya tarehe 14.04.2012

Haya ni mabo ambayo uongozi umepata baraka kutoka kwa waanachama kujadili na kuja na majibi kwenye kikao kinachokuja cha tarehe 01.04.2012

mwisho nitoe tena shukrani zangu za dhati kwa uongozi kwa kazi nzuri wanayoifanya kuanzia kwa katibu na msaidizi wake, muweka hazina na msaidizi wake, makamu mwenyekiti wangu na viongozi wa kamati zetu za chama, tuenedelee kuwa na umoja, nidhamu na juhudi tunayoionyesha ili hazima na malengo ya chama yatimie!

imetolewa 05032012
Na Japhet mukala
Mwkt wa chama