UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Monday, December 12, 2011

UTARATIBU WA KUTOA HOJA BINAFSI

Kutokana na ukweli halisi wa chama chetu kufuata misingi ya haki na usawa kwa wanachama wetu, uongozi unatoa nafasi kwa mwanachama yeyeto yule ambaye amehudumia chama kwa zaidi ya miezi sita (Probation period) , kutoa dukuduku lake kwa njia yoyote iwe moja kwa moja kwa uongozi au kwa njia ya barua, na kama ilivyo ada, kila mwisho wa vikao vyetu vya jumapili ya mwanzo wa mwezi huwa tunatoa muda wa maswali na majibu kuhusu jambo lolote linalohusu chama, lengo la nafasi hii ni kutoa ushiriki mpana kwa mjumbe kuondoa dukuduku lolote juu ya jambo amabalo analiona sio sawa au anaweza kuwa anataka ufafanuzi au anashauri au anataka maelezo toka kwa mjumbe mwenzake au kwa uongozi, na kama mjumbe amadhamilia kutoa hoja nzito yenye maslahi kwa chama, anashauriwa awasiliane na uongozi mapema iwezekanavyo ili uongozi upate nafasi ya kuipitia hoja yake na kuangalia uwezekano wa kuipatia muda kwenye ajenda za mkutano unaofata, lakini pili kuona kama hoja mezani ina usahihi na uhalali wa kujadiliwa kwa maslahi ya chama.

tunaomba sana ushiriki wenu na mawazo yenu ili kuboresha chama na kutimiza malengo yetu kwa wakati
imetolewa na

Japhet Mukala
mwenyekiti wa chama
12122011

No comments: