UONGOZI MPYA WA CHAMA 2016/17

Japhet Mukala -Mwenyekiti wa chama

Johanes Mujuni-Makamu mwenyekiti

Denice Kahangwa-Katibu mkuu wa chama

Nelson Ntoroma-Naibu Katibu mkuu

Elizeus Izoba-Mweka hazina wa chama

Agnetha Byashalila- Muweka hazina msaidizi

Hamidu Mabaraza-Msemaji mkuu wa chama

Monday, December 19, 2011

WAKATI TUNAJIANDAA KUSHEREHEKEA SIKU KUU YA XMAS



Ndugu wanachama,

Namshukuru mwenyezi mungu kwa kutuwezesha kufika hapa leo tukiwa wazima wa afya, ni rehema yake tu kuona hadi leo tunavuta pumzi yake,inabidi tumshukuru sana na kumtukuza  Mwenyezi kwa kutenda yaliyo mema kila wakati.

Kwa niaba ya chama cha vijana wa kanyigo, napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza na kuwatakia sikuu njema yenye furaha na matumaini katika maadhimisho ya kuzaliwa kwake yesu kristo, ni furaha sana na ni siku muhimu ya kutafakari matendo yetu, kujiuliza sababu hasa ya kuzaliwa kwake yesu, kama ilikuwa kwa ajili ya dhambi zetu je tunayatekeleza yale aliyotwambia kuyafuata yale aliyotuachia kama urithi sahihi wa kuuona ufalme wa mbingu, tujiulize ndani ya kipindi chake cha kuhudumu cha miaka mitatu je alitimiza yale yote aliyokusudia kufanya hapa duniani duniani?kama sio yote ni nani anatakiwa kuyakamilisha yale yaliyokusudia na ni kwa jinsi gani tunaweza kuyakamilisha na kwa msaada wa nani? ni nini alitwambia kufanya juu wa ufalme wa mbingu?

Nadhani ni maswali magumu sana, inahitaji muda mwanana, busara na wigo mpana katika kutafakari majibu yake wakati huu wa maadhimisho na baada ya maadhimisho, tusherehekee kwa taadhari na tafakari yenye tafakuri timilifu, na upembuzi yakinifu juu ya matendo na matakwa yampasayo mwanadamu kuyafata ili awe mkiristu aliye na haki mbele za mungu na kwa njisi gani mwanadamu anaweza kuwa na haki mbele yake aliye juu.

Mwisho niwatakie sherehe na baraka njema pamoja na familia zetu kwa ujumla
Tukumbuke kuwaombea walio kwenye mateso mbalimbali, walio wagonjwa, walio na njaa, waliohukumiwa, waliokosa matumaini, waliosafarini, hata wasioamini juu ya wokovu wa mungu., waliombali na familia zao, walio vitani, wanaopambana na uovu kila kukicha. Mungu ni mwema siku zote!

imani zetu ziwe ndani ya utatu mtakatifu yani, ''mungu baba, mungu mwana na roho mtakatifu'' amina
Imetolewa leo 19122011  na
Japhet Mukala

WISH U A MERRY XMASS

 

1 comment:

Anonymous said...

NI MUDA MUAFAKA WA KUJITAYARISHA NA KUTUBU DHAMBI ZETU ILI TUZALIWE UPYA!